United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania
Mheshimiwa Spika,leo hii tunafikia tamati ya Mkutano wa Kumi na Mbili wa Bunge lako Tukufu ambao ulianza Kikao chake cha kwanza tarehe 4 Septemba 2018. Hivyo, hatunabudi kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kuhitimisha shughuli zote zilizopangwa kwenye Mkutano huu tukiwa na afya njema.