United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Y. Ndugai (Mb) anasikitika
kutangaza kifo cha Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Mhe. Dkt. Elly Marko Macha kilichotokea katika Hospitali ya New Cross, Wolverhampton nchini Uingereza alikokuwa akipatiwa matibabu.
Mipango ya
Kusafirisha Mwili wa Marehemu kuja nchini ikiwa ni pamoja na taratibu za
mazishi inaendelea kufanywa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na Familia ya
Marehemu.
Kufuatia Msiba huu. Mhe. Spika ameahirisha vikao vya kamati vilivyokuwa vinaendelea leo hadi kesho Jumamosi tarehe 1 Aprili, 2017.
Taarifa zaidi juu ya Msiba huu zitaendelea kutolewa na Ofisi ya Bunge kadri zitakavyopatikana.
“Mwenyezi
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi.” AMINA
Hon. Shabani Hamisi Taletale
Morogoro Kusini Mashariki (CCM)