Parliament of Tanzania

TAARIFA YA MHE. SPIKA JUU YA MISWADA ILIYOPITISHWA NA BUNGE KATIKA MKUTANO WA TISA NA KUSAINIWA NA MHE. RAIS KUWA SHERIA

TAARIFA YA MHE. SPIKA

________________

[Imetolewa Chini ya Kanuni ya 33(1) ya Kanuni za

Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016]

_______________

Katika Mkutano wa Tisa wa Bunge, Bunge lilipitisha Miswada Minne ya Sheria ya Serikali ifuatayo:-

1. Muswada wa Sheria ya Shirika la Mawasiliano Tanzania wa Mwaka 2017 [The Tanzania Telecommunications Corporation Bill, 2017];

2. Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 4) wa Mwaka 2017 [The Written Laws (Miscellaneous Amendment) (No. 4) Bill, 2017];

3. Muswada wa Sheria ya Wakala wa Meli Tanzania wa Mwaka 2017 [The National Shipping Agencies Bill, 2017]; na

4. Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya wa Mwaka 2017 [The Drugs Control and Enforcement (Amendment) Bill, 2017].

Kwa taarifa hii, napenda kuliarifu Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Miswada hiyo minne imepata Kibali cha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa Sheria za Nchi zinazoitwa:-

1. Sheria ya Shirika la Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya Mwaka 2017 [The Tanzania Telecommunications Corporation Act No.12 of 2017];

2. Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 4) Na. 13 ya Mwaka 2017 [The Written Laws (Miscellaneous Amendment) (No. 4) Act No.13 of 2017];

3. Sheria ya Wakala wa Meli Tanzania Na. 14 ya Mwaka 2017 [The National Shipping Agencies Act No. 14 of 2017]; na

4. Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Na. 15 ya Mwaka 2017 [The Drugs Control and Enforcement (Amendment) Act No. 15 of 2017).

Job Y. Ndugai (Mb)

SPIKA

30 Januari, 2018

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's